
Wataalamu wa Kodi Afrika Mashariki Wakutana Zanzibar
Na Muandishi Wetu. MAMLAKA za Kodi za nchi za Afrika Mashariki, zimesema zitaendelea kushirikiana pamoja katika kutatua changamoto za kodi zinazofanana na kubadilishana uzoefu ambao utasaidia kuimarisha mapato ya nchi zao. Kaimu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA) Ndg. Saidi Ali Mohamed, alieleza hayo leo wakati akifungua mkutano wa 98 wa Kamati ya Wataalamu wa Mamlaka za Mapato za Afrika Mashariki ulioanza leo katika Ukumbi wa Hoteli ya Madinat Al Bahr iliyopo Mbweni nje kidogo ya mji wa Zanzibar. Kamishna Said alisema watahakikisha wanajadiliana na kushirikiana katika kutafuta mbinu ambazo zitawezesha kutumiwa na nchi hizo




